Na.Sylvester Onesmo wa Jeshi la Polisi Dodoma. Jeshi la Polisi Mkoa
wa Dodoma limeendelea kufanya msako katika maeneo mbalimbali na
kufanikiwa kuwakamata wanawake wapatao 15 wanaojihusisha na biashara
haramu ya kuuza miili yao kutoka mikoa mbalimbali nchini. Msako huo
ulifanyika tarehe 05/02/2014 majira ya 21:00hrs katika mitaa ya uhindini
na Air Port.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi DAVID MISIME - SACP amewataja watu hao kuwa ni:
1. VERONICA D/O JOEL mwenye miaka 23, Mnyakyusa mkazi wa Sai Mbeya.
2. ROSE D/O MICHAEL mwenye miaka 30, Mgogo, Mkazi wa Kikuyu Dodoma.
3. MARIAM D/O JORDAN mwenye miaka 26, Mhehe mkazi wa Tukuyu Mbeya.
4. REHEMA D/O RAMANDANI mwenye miaka 38, Mlugulu mkazi wa Airport Morogoro.
5.JOYCE D/O MARTINE mwenye miaka 22, Mnyamwezi mkazi wa Chinangali West Dodoma.
6. FATIA D/O SARATIELI mwenye miaka 20, Mgogo mkazi wa Makanda Bahi Dodoma.
7. BOKE D/O CHACHA mwenye miaka 27, Mkurya mkazi wa Tarime Mara.
8. SWAUMU D/O BAKARI mwenye miaka 23, Mnyamwezi mkazi Chinangali Dodoma.
9. ROSS D/O MASAKI mwenye miaka 28, Mchaga mkazi wa Sanya juu Moshi.
10. SCOLASTIA D/O COSTANTINO mwenye miaka 22, Mnyakyusa mkazi wa Gongolamboto Dar es salaam.
11. HAPPY D/O JULIUS mwenye miaka 31, Mnyamwezi mkazi wa Urambo Tabora.
12. AISHA D/O HASSAN mwenye miaka 38, Mbulu mkazi wa Babati Manyara.
13.JULIANA D/O DOMINICK Mwenye miaka 31, Mnyakyusa, mkazi wa Airport Dodoma.
14.DATIVA D/O LUKWEMBE mwenye miaka 29, Mhaya mkazi wa Kiziba Bukoba Kagera.
15.DORIN D/O MASSAWE mwenye miaka 23, Mchaga mkazi wa Kiboshomaro Moshi.
Aidha Kamanda MISIME amesema katika msako huo watu wawili wanaume
walikamatwa wakiwa na mirungi robo kilo katika mtaa wa barabara ya nane
(8) Manispaa ya Dodoma ambao ni NASSOR S/O ALLY mwenye miaka 45, Mwarabu
mkazi wa barabara ya kumi na AYUBU S/O TEPO mwenye miaka 40, Muarusha,
Fundi cherehani mkazi wa Chamwino.
Pia huko katika Wilaya ya Kongwa
kijiji cha Mlanje kata ya Matongoro Tarafa ya Zoisa alikamatwa mtu
mmoja aliyefahamika kwa jina la SHEDRACK S/O MACHILE mwenye miaka 46,
Mgogo, Mkulima akiwa na Lita 30 za pombe ya moshi akiziuza.
Kamanda MISIME amesema msako unaendelea na amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi
Tafuta katika Blogu Hii
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo EKILI ONE. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo EKILI ONE. Onyesha machapisho yote
Alhamisi, 13 Machi 2014
SAMWELI SITA AULA BUNGE LA KATIBA
LOWASSA AIKANA NOTI YA SH 500 YENYE PICHA YAKE BADALA YA RAIS.
Kumekuwa
na muendelezo wa matukio kadhaa kutoka kwa kikundi cha watu kumuhusisha
Mhe. Edward Lowassa na matukio ya uongo na kumzushia vitu vya ajabu
kabisa, hususani katika mitandao ya kijamii.
Kumesambazwa picha ya noti ya shilingi mia tano yenye picha ya Mhe. Lowassa. Kitendo hicho siyo utani, bali ni dhihaka na dharau kwa alama za Utaifa na Mamlaka ya nchi. Lowassa Amesema hajui na wala ahusiki na usambazaji wa Noti hiyo Mitandaoni
Mhe. Lowassa anaheshimu maoni ya watu na nguvu ya mitandao ya kijamii, lakini anasisitiza umuhimu kwa wananchi kutumia nguvu hiyo ya mitandao kwa kujadili maendeleo ya nchi yetu badala ya kuwa watu wa kuzusha mambo yasiyo na tija kwa nchi yetu.
Imetolewa na:
Ofisi ya Mhe. Lowassa (MB)
Kumesambazwa picha ya noti ya shilingi mia tano yenye picha ya Mhe. Lowassa. Kitendo hicho siyo utani, bali ni dhihaka na dharau kwa alama za Utaifa na Mamlaka ya nchi. Lowassa Amesema hajui na wala ahusiki na usambazaji wa Noti hiyo Mitandaoni
Mhe. Lowassa anaheshimu maoni ya watu na nguvu ya mitandao ya kijamii, lakini anasisitiza umuhimu kwa wananchi kutumia nguvu hiyo ya mitandao kwa kujadili maendeleo ya nchi yetu badala ya kuwa watu wa kuzusha mambo yasiyo na tija kwa nchi yetu.
Imetolewa na:
Ofisi ya Mhe. Lowassa (MB)
Jumamosi, 8 Februari 2014
WANA NCHI WA TABORA WATOA KERO ZAO JUU YA MAWASILIANO
WANANCHI wa kata za Loya na Lutende katika wilaya ya Uyui
mkoani Tabora wametoa kilio chao kwa Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia
Prof Makame Mbarawa, wakimwomba
kuwatatulia kero yao ya siku nyingi kwa kuwawekea mnara wa mawasiliano
kwa ajili ya kupata huduma za simu za mkononi.
Kilio hicho wamekitoa mbele ya Mbunge wa Jimbo la Igagula
Dk Athuman Mfutakamba wakati wa ziara yake ya siku nne katika jimbo hilo ya
kukagua utekelezaji wa ilani ya chama cha Mapinduzi pamoja na miradi mbali
mbali ya maendeleo ya wananchi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Wananchi hao wamesema kata
hizo ni miongoni mwa kata ambazo hazina mawasiliano ya aina yeyote ile katika
jimbo la Igalula kutokana na kutokuwa na mnara hata mmoja wa kuwasaidia kufanya
mawasiliano hivyo kuwafanya wananchi hao kuwa nyuma kimaendeleo.
Wamebainisha kuwa kilio hicho cha kuomba kuwekewa minara
kimekuwa ni cha siku nyingi na hakijapatiwa ufumbuzi zaidi ya kupewa
ahadi hewa mbunge wao kila mara, hali
inayowafanya baadhi yao kuichukia serikali ya chama cha mapinduzi kwa kuona
kuwa haiwajali wananchi wake lakini kumbe wapi jamani.
Diwani wa kata ya Lutende Bwana Pancras Luge amesema Kilio
cha wananchi wake ni mnara wa mawasiliano, na kwamba hapa hawawezi kuongea na
simu hata kama kuna tukio la mauaji kama si kukanyaga baiskeli kwenda kutoa
taarifa sehemu husika.
Luge amesema hivi sasa hawezi kupita barabarani kifua mbele
kwani amekuwa akitukanuwa sana na wananchi kutokana na kukosekana kwa
mawasiliano hayo ya Simu.
Akijibu tuhuma za wananchi dhidi yake Mbunge wa Jimbo hilo Dk Athuman Mfutakamba
amesema Serikali tayari imeshatenga fedha kwa ajili ya minara hiyo na
mkandarasi tayari yupo na kuongeza kuwa yeye kama mbunge wao atafanya mawasiliano
na Waziri anayehusika ili kuhakikisha wananchi wa Loya na Lutende wanapata
mawasiliano ya simu za mkononi.
Nikiripoti kutoka wilaya ya Uyui mimi ni dikodiko.nyagale
JAMBAZI ARIYE KUWA AKIENDESHA MAUAJI MKOANI MAARA ATIWA MBARONI NA POLICE
Jambazi aliye itikisa tarime kwa mauaji ametiwa mikononi mwa police akiwa amekimbilia mkoani tanga
pia na mwenzake kuawa na jeshi la police kikosi cha kanda maalum akiwa ameachiwa bunduki aina ya Cmg
pia police wanaenderea na mahojiano zaidi ilikujua alikuwa analengo gani.
pia na mwenzake kuawa na jeshi la police kikosi cha kanda maalum akiwa ameachiwa bunduki aina ya Cmg
pia police wanaenderea na mahojiano zaidi ilikujua alikuwa analengo gani.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)