Tafuta katika Blogu Hii

Jumamosi, 8 Februari 2014

WANA NCHI WA TABORA WATOA KERO ZAO JUU YA MAWASILIANO



WANANCHI wa kata za Loya na Lutende katika wilaya ya Uyui mkoani Tabora wametoa kilio chao kwa  Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia Prof  Makame Mbarawa, wakimwomba  kuwatatulia kero yao ya siku nyingi kwa kuwawekea mnara wa mawasiliano kwa ajili ya kupata huduma za simu za mkononi.

Kilio hicho wamekitoa mbele ya Mbunge wa Jimbo la Igagula Dk Athuman Mfutakamba wakati wa ziara yake ya siku nne katika jimbo hilo ya kukagua utekelezaji wa ilani ya chama cha Mapinduzi pamoja na miradi mbali mbali ya maendeleo ya wananchi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Wananchi hao wamesema kata hizo ni miongoni mwa kata ambazo hazina mawasiliano ya aina yeyote ile katika jimbo la Igalula kutokana na kutokuwa na mnara hata mmoja wa kuwasaidia kufanya mawasiliano hivyo kuwafanya wananchi hao kuwa nyuma kimaendeleo.

Wamebainisha kuwa kilio hicho cha kuomba kuwekewa minara kimekuwa ni cha siku nyingi na hakijapatiwa  ufumbuzi zaidi ya kupewa ahadi hewa mbunge wao  kila mara, hali inayowafanya baadhi yao kuichukia serikali ya chama cha mapinduzi kwa kuona kuwa haiwajali wananchi wake lakini kumbe wapi jamani.

Diwani wa kata ya Lutende Bwana Pancras Luge amesema Kilio cha wananchi wake ni mnara wa mawasiliano, na kwamba hapa hawawezi kuongea na simu hata kama kuna tukio la mauaji kama si kukanyaga baiskeli kwenda kutoa taarifa sehemu husika.

Luge amesema hivi sasa hawezi kupita barabarani kifua mbele kwani amekuwa akitukanuwa sana na wananchi kutokana na kukosekana kwa mawasiliano hayo ya Simu.

Akijibu tuhuma za wananchi dhidi yake  Mbunge wa Jimbo hilo Dk Athuman Mfutakamba amesema Serikali tayari imeshatenga fedha kwa ajili ya minara hiyo na mkandarasi tayari yupo na kuongeza kuwa yeye kama mbunge wao atafanya mawasiliano na Waziri anayehusika ili kuhakikisha wananchi wa Loya na Lutende wanapata mawasiliano ya simu za mkononi.

Nikiripoti kutoka wilaya ya Uyui mimi ni dikodiko.nyagale

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

mwanga wetu maoni