Tafuta katika Blogu Hii

Jumamosi, 26 Oktoba 2013

MSANI WA TABORA LIZZ DADY ACHEMSHA FIESTA SUPER NYOTA 2013

LIZZ DADY | Mshindi super nyota fiesta 2013 Tabora [PICHA HAIHUSIANI NA TUKIO]

Msanii huyu ameuambia mtandao huu kuwa upatikanaji wa mshindi haumpi tu wasiwasi ila hakuna chochote walichokifanya kumpata mshindi huyo wa SUPER NYOTA ambapo Liz Dady amedai kuwa hata mashabiki waliona na kutambua ushindi kuwa haukustahili kwenda hata kwa huyo mshindi wa kwanza na wapili. Akijigusia yeye mwenyewe, amesema hata kama hakustahili kuwa yeye lakini si kwa ushindi walioutoa kwa mshindi waliyempanga wao.

"Mimi niling'ara jukwaani kiasi cha mashabiki kunitaka nirudi jukwaani, si mimi tu niliyetisha kwa jukwaa ila pia jamaa mmoja wa Shinyanga pia aling'ang'aniwa na mashabiki kwa uwezo alouonesha.... kupitia mengi yaliyojiri pale yalinifanya niaamini kuwa mshindi amepangwa, sikatai kushindwa lakini mziki hauendi hivyo kwani mwisho mashabiki ndio watakao zisikiliza kazi zao na kama watazirusha hizo battle radioni utapata nguvu ya kujua ninachokiongea na utaweza kukijaji" Alisema Liz Dady

Mashindano hayo yamefanyika jana usiku tarehe 25/10/2013 club sansiro jijini dar. Kinachouma kama kweli wamechakachua, je mziki utaendelea kweli?

Maoni 1 :

mwanga wetu maoni